1st August, 2018
Wakati mdahalo wa ajenda nne kuu za serikali ya jubilee ukizidi kushika kasi darubini inasalia katika mojawapo ya malengo haya hii ikiwa ni sekta ya afya. Nafasi ya wanafamasia au ukipenda wataalam katika nyanja ya dawa inaanza kuonyesha utepetevu wa hali ya juu ikibainika wazi kuwa huenda serikali haijazingatia barabbara nafasi ya wataalam hawa.