.
1st August, 2018
Maafisa wa usalama katika mtaa wa Kayole wanachunguza kisa cha wanafunzi kumi wa shule ya msingi ya Dhawabu wanaodaiwa kufumaniwa katika nyumba moja mtaani Kayole wakijihusisha na tendo la ngono. Tukio ambalo sasa linaibua mjadala kuhusiana na maadili ya watoto katika jamii na haswa katika nyakati za leo huku usimamizi wa shule ukidhibitisha kupokea madai hayo na kwamba uchunguzi umeanza.