.
26th July, 2018
Kifaru mwingine ameripotiwa kufa na kufikisha idadi ya vifaru waliokufa baada ya kuhamishwa katika mbuga ya wanyama ya tsavo kuwa kumi. Akitoa ripoti kamili kuhusiana na kilichosababisha maafa ya vifaru hao waziri wa utalii Najib Balala amewapiga kalamu maafisa sita wa shirika la huduma kwa wanyama pori kwa kile alichokitaka kuwa utepetevu katika utendakazi wao.