.
23rd July, 2018
Wanaume wawili wamefariki walipokuwa kazini kwenye mgodi mmoja kijijini Getare, eneo bunge la bonchari kaunti ya kisii. Douglas Ratemo na Daniel Okero wote wenye umri wa miaka thelathini na mitano waliangukiwa na mwamba ulioporomoka kwenye timbo hilo na kuwafunika. Usalama wa wachimba migodi katika timbo hilo umezungumziwa kwa masikitiko baada ya mkasa huo Uliowapokonya uhai marafiki wawili ambao wamekuwa wakitegemea riziki katika eneo hilo.