23rd July, 2018
Shughuli ya kuwafurusha watu kutoka msitu wa mau unaendelea kuibua hisia kali seneta wa Kericho Aaron Cheruiyot akimkashifu vikali katibu mkuu wa Jubilee ambaye pia ni waziri Raphael Tuju kwa madai kwamba anashabikia unyama unaotumiwa kuwafurusha. Haya yanajiri huku baadhi ya wakaazi wa narok wakiandamana kushinikiza shughuli hiyo iendelee.