22nd July, 2018
Washukiwa 99 wa wizi wa mafuta wamekamatwa katike eneo la barabara ya lunga lunga hapa jijini Nairobi katika operesheni ambayo imeendeshwa na maafisa wa polisi kwa ushirikiano na shirika la uhifadhi mazingira nchini NEMA pamoja na tume ya kudhibiti kawi E.R.C. Kadhalika maelfu ya lita za mafuta yalinaswa kisha matanki ya mafuta hayo kuharibiwa. Inaarifiwa kuwa washukiwa hao wanaiba mafuta hayo na kisha kuyachanganya na bidhaa zingine kabla ya kuwauzia wateja