.
12th July, 2018
Viongozi kutoka eneo la magharibi ya Kenya sasa wanamtaka kiongozi wa mashitaka ya umma na mkurugenzi wa idara ya upelelezi kumkamata na kuanzisha mashtaka dhidi ya aliyekuwa Gavana wa Nairobi Evans Kidero kwa kile wanachodai alifuja mabilioni ya fedha katika kampuni ya sukari ya Mumias. Kulingana na viongozi hao, Kidero aliangusha kampuni ya Mumias Sugar na kuwaacha wakulima wa miwa wakiwa maskini alipokuwa mkurugenzi mkuu katika kampuni hiyo.