11th July, 2018
Zaidi ya maskwota mia tisa katika eneo la Kisauni wametoa wito kwa idara ya mahakama kusitisha shughuli zozote kuendelea katika kipande cha ardhi ya Ekari 132 inayokumbwa na mzozo katika eneo hilo. Maskwota hao wamelalama kwamba kesi waliowasilisha mahakamani imechukuwa muda kutatuliwa na tayari ardhi hiyo imeanza kuuzwa.