4th July, 2018
Mkuu wa mashtaka ya umma Noordin Haji ameagiza kukamatwa na kufunguliwa mashataka bwana Patel Mansukh na meneja wake Vinoy Jaya-Kumar kwa makosa ya kuua bila kukusudia. Aidha maafisa kadhaa wa NEMA na warma wamewekwa kwenye orodha ya kufunguliwa mashtaka inayohusiana na kuitelekeza kazi hatua iliosababisha bwawa la Patel kuvunja kuta zake na kusabisha vifo vya watu arobaini na saba.