2nd July, 2018
Muungano wa wawakilishi wa wadi kote nchini umekutana kutoa taarifa kwa vyombo vya habari kuhusiana na usalama wa waakilishi wadi. Wakiongozwa na spika wa kaunti ya Kajiado Johnson Osoi ambaye pia ndiye mwenyekiti wa muungano huo walisema kuwa wakati umefika kwa serikali kutoa usalama wa kutosha kwa waakilishi wadi wote kama waheshimiwa wengine. Haya yanajiri saa chache baada ya mwakilishi wadi wa silale nelson lotela kupatikana akiwa mzima baada ya siku moja ya kutoweka katika hali tatanishi.