28th June, 2018
Watu kumi na watano wamethibitishwa kufariki katika mkasa wa moto ulioteketeza majengo yaliyo karibu na soko la gikomba hapa jijini nairobi usiku wa kuamkia leo. Kadhalika watu sabini wanaendelea kupokea matibabu katika hospitali ya rufaa ya kenyatta baada ya kujeruhiwa katika mkasa huo. Bado haijabainika ni nini kilichosababisha moto huo.