27th June, 2018
Wabunge wa zamani kutoka eneo la mlima Kenya wameunga mkono juhudi za rais Uhuru Kenyatta kukabiliana na ufisadi. Wabunge hao wakiongozwa na aliyekuwa mbunge wa Mukurweini Kabando wa Kabando, walikutana na kiongozi wa upinzani Raila Odinga na baadaye kuzungumza na wanahabari. Kabando amewaonya wanaozungumzia siasa za 2022 kukoma, akisema kuwa huu ni wakati wa kutumikia wananchi.