21st June, 2018
Kitengo cha kuchunguza ajali za ndge nchini sasa kinakisia huenda maagizo ya kumtaka rubani wa ndege aina ya Cessna Caravan kubadilisha njia na kupitia mlima wa Aberdare badala ya kupitia mlima wa Ngong yalihitilafiana na safari nzima ya ndege hiyo iliyoanguka na kusababisha vifo vya watu kumi papo hapo. wakizungumza wakati wa taarifa ya pamoja wizara ya uchukuzi sawa na halmashauri ya ndege nchini wamesema hata hivyo uchunguzi ungali unaendelea.