.
21st June, 2018
Mbunge wa Malindi Aisha Jumwa amepuuzilia mbali madai kwamba chama cha odm kinapanga kumuondoa katika kamati ya bunge ya huduma kwa huduma za bunge .Aisha amesema kuwa hajatengana na chama cha ODM na kionmgozi wa chama hicho raila odinga na kwamba ni tetesi za uongo kwenye vyombo vya habari , jumwa ametaja uhusiano wa kisiasa baada ya rais uhuru kenyatta na kiongozi wa ODM Raila Odinga umemfanya kuwa wazi kutangamana na wansiasa wengine . Aisha hata hivyo amesema kuwa atamuunga mkono William Ruto kwa kinyang'anyiro cha urais mwaka wa 2022.