14th June, 2018
Licha ya bajeti ya mwaka huu kuwasilishwa bungeni wengi wamekuwa wakifuatilia moja ya ajenda nne za serikali ya rais Uhuru Kenyatta ambayo ni makaazi. Mojawapo ikiwa ujenzi wa makaazi ya bei nafuu kupambana na ukosefu wa nyumba za kutosha. Katika kaunti ya Kakamega maafisa wa kulinda magereza bado wanaishi katika nyumba za matope.