12th June, 2018
Shule ya upili ya wasichana ya Maasai iliyoko katika kaunti ya Narok imefungwa, baada ya wanafunzi mia saba wa shule hiyo kususia masomo na kuondoka shuleni mapema leo, ili kulalamikia kile walichokitaja kuwa unyanyasaji wa jinsia na walimu wao wa kiume. Wazazi wenye hasira wamekilaani kitendo hicho na kumtaka waziri elimu, Amina Mohamed, kuingilia kati na kuwachukulia hatua walimu wote wanaohusika na kitendo hicho.?