12th June, 2018
Harakati za kutafuta majibu kuhusiana na sakata ya kupotea kwa mamilioni ya pesa katika idara ya NYS ziliendelea hii leo mahakamani. Washukiwa wa sakata hiyo kwa mara nyingine wakiachwa kwenye mataa kuhusiana na ombi lao la kuachiliwa kwa dhamana. Hata hivyo, mahakama kuu imeahirisha uamuzi wa huo hadi tarehe 19 mwezi huu.