.
9th June, 2018
Naibu rais William Ruto amezuru kaunti ya Laikipia hii leo katika hafla ambayo iliibua siasa kali za uchaguzi mkuu ujao wa 2022. Japokuwa hotuba ya Ruto ilijikita katika kuwataka wakazi wa maeneo hayo kutangamana wachangiaji katika hafla hiyo walimpigia debe kumrithi rais Kenyatta. Miongoni mwa waliohudhuria hafla hiyo ni mwakilishi wa kike wa kaunti ya Kiambu Gathoni wa Muchomba na waziri wa kilimo Mwangi Kiunjuri.