.
3rd June, 2018
Viongozi wa chama cha Jubilee kutoka sehemu mbalimbali wamemkosoa kiongozi wa NASA Raila Odinga kwa kutoa mapendekezo kuwa katiba inatakiwa kufanyiwa marekebisho wakidai kuwa ana njama fiche. Wakizungumza katika kanisa katoliki la St. Trizer huko Kiambu wamedai kuwa Jubilee haimwamini Raila. Matamshi yao yanatukia huku kukiwa na mpangilio maalum wa utendakazi kati ya Raila Odinga na rais Uhuru Kenyatta kupitia kwa jopo la watu kumi na wanne lililobuniwa.