.
24th May, 2018
Kituo cha Radio Maisha kinachomilikiwa na shirika la habari la Standard kinaadhimisha miaka minane tangu kuanzishwa rasmi mwaka 2010. Hafla ya kipekee ya kuadhimisha hatua hii imefanyika katika makao makuu ya shirika hili, kilele chake kikiwa ukataji keki. Kaimu afisa mkuu mtendaji wa Standard Group, Orlando Lyomu, ametaja maadhimisho haya kuwa ya kipekee.