23rd May, 2018
Shirika la Standard Group limetia mkataba wa maelewano na taasisi ya wahasibu wa umma nchini ICPAK.mwenyekiti wa taasisi hiyo Julius Mwatu alisema makubaliano hayo yanalenga kuboresha utendakazi wa taasisi ya uhasibu nchini na wanachama kufahamu mengi kuhusu taaluma na mikakati inayofanywa kuboresha matakwa ya wahasibu nchini. Wakizungumza huko Mombasa ICPAK ilikubali kuendeleza ushirikiano mwema na gazeti la Standard na kuahidi kuendelea kusoma gazeti hilo kila mara ili kufahamu mengi yanayojiri nchini.