.
20th May, 2018
Gavana wa Tharaka Nithi Muthomi Njuki amepongeza kupitishwa kwa sheria ya kuthibiti matumizi ya tarakilishi na kukabili uhalifu wa mitandao. Akizungumza baada ya kuzindua matembezi ya wanafunzi wa shule za msingi na upili Njuki amesema kuwa sheria hiyo itawazuia vijana kutumia mitandao visivyo. Njuki amesema kuwa baadhi ya vijana wamekuwa wakitumia mitandao kuwa jukwaa la kuwashambulia watu jambo ambalo huzua migawanyiko.