.
13th May, 2018
Gavana wa Mandera Ali Roba amekosoa hatua ya serikali kuu kufunga timbo za eneo hilo kwa kigezo cha ugaidi katika eneo hilo. Gavana Roba aliyezungumza baada ya kuzindua shughuli ya upanzi wa miti katika kaunti ya Mandera, amesikitika kwamba hatua hiyo itarudisha nyuma maendeleo ya sehemu hiyo, akiwataka wadau wa asasi za usalama kubuni mbinu za kudumu katika kupambana na ugaidi nchini.