.
15th April, 2018
Naibu rais William Ruto ameendelea kujipata lawamani kutoka kwa wabunge wa NASA ambao wanamshutumu kwa kile wanadai ni njama yake ya kusambaratisha juhudi za utangamano, zinazoendeshwa na rais Uhuru Kenyatta na kiongozi wa nasa Raila Odinga. Wabunge hao wanadai msimamo wa Ruto dhidi ya marekebisho ya katiba unavunja moyo.