.
4th April, 2018
Rais Uhuru Kenyatta amewaonya maafisa wa umma wanaofuja pesa za umma akisema serikali haitawavumilia watu wanaolemaza juhudi za kuafikia maendeleo. rais amewaonya wale wanaoendeleza siasa akisema muda wa siasa umekwisha. Rais aliyeandamana na naibu rais William Ruto pamoja na viongozi wengine wa Rift Valley alikuwa akizungumza alipozindua hospitali ya kisasa ya macho katika hospitali ya Tenwek kaunti ya Bomet. Aidha rais ametoa muda wa mwaka mmoja kwa hospitali za rufaa nchini kujenga vitengo vya matibabu ya macho na meno.