28th March, 2018
Kwa siku ya tatu, wakili anayekumbwa na utata Miguna Miguna ameendelea kuzuiliwa na maafisa wa serikali baada ya kuzuiliwa kuingia nchini alipowasili kutoka nchini Canada. Waziri wa usalama Fred Matiang'i, Inspekta mkuu wa polisi Joseph Boinnet na mkurugenzi wa uhamiaji Gideon Kihalangwa wamekosa kufika mahakamani kama walivyoagizwa kufuatia utata unaogubika kuzuiliwa kwa Miguna Miguna. Jaji George Odunga alitoa agizo jipya kutaka polisi kumuwasilisha Miguna mahakamani.