.
20th March, 2018
Seneta wa Bungoma Moses Wetangula amebanduliwa kutoka nafasi ya kiongozi wa waliowachache katika bunge la Seneti. Maseneta wote kumi na nane waliokuwa wamehudhuria mkutano huo wakiafikiana kwa pamoja kumng’atua Seneta Wetangula. Haya yanajiri huku vyama vya ANC, Wiper na Ford Kenya wakituhumu ODM kuendeleza shinikizo dhidi ya Wetangula.