.
12th March, 2018
Wakazi wa eneo bunge la Bahati kaunti ya Nakuru wanalitaka bunge kufanya hima kupitisha na kuhakikisha utekelezaji wa mswada kuhusu Kawi uliopendekezwa. Wanasema mswada huo uliasisiwa na Seneta wa Baringo Gideon Moi utasaidia pakubwa katika kuwanufaisha na raslimali zilizo katika eneo hilo. Walikuwa wakizungumza kwenye kikao cha umma kuhusu mswada huo.