.
22nd February, 2018
Mwili wa akwilina akwilini, mwanafunzi aliyeuawa kwa risasi nchini Tanzania katika vurugu za maandamano kati ya wafuasi wa chama kikuu cha upinzani na polisi nchini Tanzania, umeagwa leo mjini Dar es salaam katika ibada maalumu iliyowaleta viongozi, wanasiasa, na wote walioguswa na kifo chake. Kifo cha mwanafunzi huyo mwenye umri wa miaka 22 kimeibua mjadala wa kitaifa kuhusu ubabe wa polisi dhidi ya raia na mfululizo wa visa vya mauaji, utekaji na kupotea kwa raia wa taifa hilo.