.
19th February, 2018
Washukiwa wawili wa wizi wamekamatwa katika eneo la Kikuyu baada ya jaribio lao la kumnyang`anya hela mhudumu wa kituo cha mafuta kutibuka. Wawili hao waliokuwa wakiendesha pikipiki nusra wauawe na wakaazi waliokuwa na gadhabu. Maafisa wa polisi waliokuwa wakishika doria waliwaokoa na kuwapeleka katika kituo cha polisi cha Kikuyu. Washukiwa hao walipatikana na bunduki bandia. Visa vya wizi kwa kutumia pikipiki katika eneo la Kikuyu vimeongezeka na maafisa wa polisi wameahidi kukabiliana na wezi vilivyo.