19th February, 2018
Kikao cha umma kuhusu mauaji ya mtoto Samantha Pendo kimeanza hii leo mjini Kisumu. Hakimu mkuu mkazi wa Kisumu Beryl Omollo alitoa agizo iliyopita akisema kesi hiyo ni lazima ianze mara moja kutokana na hisia mseto zilizoibuka. Mtoto Samantha Pendo alifariki mnamo Agosti mwaka jana, baada ya kudaiwa kugongwa kichwani na polisi wakati wa ghasia zilizotokea mjini humo baada ya rais Uhuru Kenyatta kutangazwa mshindi.