15th February, 2018
Tukirejea nchini ni kuwa watu wanne wamelazwa katika hospitali ya rufaa ya Wajir baada ya familia mbili za wafugaji kuzozana kutokana na lishe na maji katika eneo bunge la Wajir mashariki. Viongozi wa eneo hilo wakiongozwa na mbunge Rashid Kasim wameshutumu tukio hilo huku wakitaka maafisa wa usalama kuanzisha uchunguzi kuhusiana na tukio hilo.