15th February, 2018
Kesi kuhusu kufurushwa kwa Miguna Miguna nchini inaendelea kutia uzito wa maagizo ya mahakama kwenye mizani, jaji Luka Kimaru akiharamisha hatua ya kutimuliwa kwake nchini. Haya yakitokea wakati jaji mkuu David Maraga akijipata kwenye hafla moja na inspekta jenerali wa polisi Joseph Boinett anayekabiliwa na tuhuma za kukaidi amri za mahakama.