14th February, 2018
Wakristo wakatoliki kote ulimwenguni wamejumuika kanisani kuadhimisha jumatano ya majivu inayoashiria mwanzo wa siku arobaini za kujinyima. Msimu huu unaofahamika kama kwaresima huwajumuisha wakatoliki katika nguzo tatu muhimu: kufunga, kuomba zaidi na kuwasaidia wasiojiweza. Papa Francis ametoa ujumbe wa kutubu dhambi, kutoa na kupokea msamaha ili kuungana na kuishi kama ndugu. Hayo yanajiri huku waumini wa kanisa katoliki wakihudhuria misa katika makanisa mbalimbali kama vile Holy Family Basilica miongoni mwa makanisa mengine kote nchini.