.
8th February, 2018
Jamii ya Wataveta sasa imeiomba serikali ya kaunti ya Taita Taveta na ile ya taifa, kutowabagua watu kutoka jamii hiyo katika mchakato wa ajira na uajiri. Kundi la wataalam kutoka jamii hiyo, linadai kutokana na uchache wao, hawajakuwa wakichukuliwa kwa uzito ima na serikali ya kaunti ama ile ya taifa.