6th February, 2018
Jaji wa mahakama kuu Luka Kimaru ameagiza kuachiliwa kwa kiongozi wa vuguvugu la NRM Miguna Miguna aliyekuwa akizuiliwa tangu Ijumaa iliyopita. Kwenye uamuzi wake, Jaji Luka Kimaru amesema amethibitisha kuwa Miguna alikuwa akizuiliwa katika jengo la mahakama ya Milimani wakati wa uamuzi huo, akionekana kujibu tetesi za alikokuwa Miguna. Aidha ameagiza awasilishwe mahakamani Kajiado mnamo tarehe 14 mwezi huu akiishutumu idara ya polisi na ofisi ya mkurugenzi wa mashtaka kwa kukiuka agizo la mahakama.