×
× KTN KTN News KTN Morning Express KTN Leo Leo Mashinani The Big Story Checkpoint News Center E-Paper Lifestyle & Entertainment Nairobian Entertainment Eve Woman Travelog TV Stations KTN Home KTN News KTN Farmers TV Radio Stations Radio Maisha Spice FM Vybez Radio Enterprise VAS E-Learning Digger Classified Jobs Games Crosswords Sudoku The Standard Group Corporate Contact Us Rate Card Vacancies DCX O.M Portal Corporate Email RMS
Login
×
Show Swahili

Siku ya pili Wakenya wakosa kupokea matangazo ya habari baada ya serikali kufunga

31st January, 2018

Jioni hii na kwa siku ya pili sasa, Wakenya watasalia kukosa matangazo kutoka kwa runinga za KTN News, NTV na Citizen TV baada ya serikali kutangaza kuwa televisheni hizo zitasalia kufungwa hadi uchunguzi wanaofanya utakapokamilika. Waziri wa usalama wa kitaifa dkt Fred Matiang’i anasema sababu ya kufungwa kwa televisheni hizi ni kutokana na vyombo hivyo kukaidi agizo la serikali kuwataka kutoshiriki kile anasema ni kuchochea uapisho haramu. Matiang’i aidha amesema kuwa uchunguzi umeanzisha kuhusiana na uapisho wa raila odinga hapo jana katika bustani ya Uhuru park akisisitiza hafla hiyo ni haramu. Hapo jana, waziri matiang'i aliratibu kwenye gazeti rasmi la serikali kuwa vuguvugu la nrm chini ya muungano wa NASA ni kundi haramu. 

.
RELATED VIDEOS