.
29th January, 2018
Huku maandalizi ya mazishi ya mjane wa aliyekuwa makamu wa rais marehemu Michael Wamalwa, Yvonne yakiendelea, makavazi ya kitaifa yanasema kuwa boma hilo sasa litafanywa kuwa kama makavazi ya kitaifa. Akiongea katika boma kwenye eneo la milimani mjini Kitale, mwakilishi wa makavazi ya kitaifa kizili chole amesema kuwa hiyo itakuwa njia moja ya kuhifadhi historia ya nchi hii. Wakati huo huo viongozi kutoka eneo hilo Trans?Nzoia walitumia fursa hiyo kumpongeza Rais Uhuru Kenyatta kwa kumteua tena Eugene Wamalwa kwenye baraza la mawaziri.