27th January, 2018
Yvonne Nambia Wamalwa, mkewe aliyekuwa makamu wa rais marehemu Michael Kijana Wamalwa, atazikwa Jumamosi wiki ijayo kwenye shamba lake la milimani mjini Kitale, kaunti ya Trans Nzoia. Mwenyekiti wa kamati ya mazishi Musikari Kombo amesema kwamba ibaada ya wafu itafanyika siku ya alhamisi katika kanisa katoliki la Consolata Shrine, eneo la Westlands, jijini Nairobi. Baadaye mwili wa marehemu utapelekwa nyumbani kwake mtaa wa Karen, Nairobi, usiku kucha kabla ya kusafirishwa kitale siku ya ijumaa. Jamaa na marafiki wanaendelea kukusanyika katika mtaa wa karen mipango ya mazishi inapoendelea. Yvonne alifariki siku ya alhamisi katika hospitali ya Nayuki Cottage alikokuwa amekimbizwa kupokea matibabu. Mwili wa mwendazake umehifadhiwa katika chumba cha maiti cha Lee. Viongozi kadha wanazidi kutoa rambi rambi zao kwa familia ya Wamalwa.