.
25th January, 2018
Maandalizi ya mazishi ya mjane wa aliyekuwa makamu wa rais nchini Michael Kijana Wamalwa, Yvonne Wamalwa yanatarajiwa kuanza baada ya mwili wake kupelekwa katika hifadhi ya maiti ya lee hapa Nairobi. Yvonne Wamalwa amefariki mapema hii leo akipokea matibabu katika hospitali ya Nanyuki cottage ambapo alipata matatizo alipokuwa kwa dadake. Viongozi mbalimbali akiwemo waziri wa maji Eugene Wamalwa wamekuwa wakifika katika hifadhi ya maiti ya lee kufarijiana.