.
24th January, 2018
Chama cha wafanyikazi wa mikahawa, hospitali, hoteli na maeneo ya burudani, KUDHEIHA, kimewataka polisi kufanya uchunguzi ili kutegua kitendawili cha madai ya wagonjwa katika hospitali ya taifa ya Kenyatta kubakwa na wafanyikazi. Katibu mkuu wa chama hicho, Albert Njeru, amesema ni kupitia uchunguzi na hatimaye kubaini vyanzo vya habari hizo ndipo ukweli na haki kwa waathiriwa vitatekelezwa.