.
23rd January, 2018
Katibu mkuu wa muungano wa vyama vya wafanyikazi nchini COTU Francis Atwoli, amehimiza haja ya mazungumzo baina ya serikali na upinzani ili kupunguza joto la siasa nchini. Akizungumza baada ya kufanya kikao na bodi ya COTU, Atwoli alionya dhidi ya wanasiasa kuendeleza misimamo mikali na kuwataka Rais Uhuru Kenyatta na raila Odinga kuzingatia mazungumzo ili kuweka mazingira bora ya biashara na maendeleo.