23rd January, 2018
Hayo yakijiri, waziri wa afya daktari Cleopas Mailu ameahidi kwamba ripoti kuhusu madai ya ubakaji katika hospitali ya Kenyatta itatolewa kwa umma hapo kesho. Akihutubu baada ya mkutano na kamati ya afya bungeni huko Mombasa, waziri Mailu amesema tayari amepokea ripoti ya uchunguzi kutoka kwa bodi ya hospitali ya Kenyatta, na kuwa anayosubiri sasa ni ripoti kutoka kwa idara ya upelelezi wa jinai.