22nd January, 2018
Bodi simamizi ya hospitali ya kitaifa ya Kenyatta sasa imeagiza kuimarishwa kwa usalama katika hospitali hiyo kufuatia tuhuma za ubakaji zilizoripotiwa na kina mama waliojifungua. Kwenye taarifa yake, bodi hiyo chini ya uongozi wa mwenyekiti Mark Bor wameagiza kuajiriwa kwa maafisa wa usalama kutoka kampuni za kibinafsi pamoja na kutoa ombi kwa polisi kuongezwa katika hospitali hiyo. aidha taarifa hiyo imeshikilia kuwa uchunguzi unaendelea kwa makini ili kubaini na kuwachukulia hatua za kisheria wahusika.