.
17th January, 2018
Wabunge wa muungano wa NASA wameafikia kutia saini hati kiapo kama hakikisho kwamba wako tayari na wanaunga mkono uapisho wa Raila Odinga na Kalonzo Musyoka. Haya yanajiri huku tetesi zikiibuka kwamba baadhi ya wanachama wa vyama tanzu wanachelea kushiriki uapisho huo. Na kama anavyoarifu Jeff Kirui chama cha Wiper kinasema kipo tayari kwa mazungumzo na upande wa Jubilee