.
17th January, 2018
Kaunti ya Mandera imepokea ripoti ya jopokazi lililobuniwa kuchunguza madai ya ufisadi kwenye idara mbalimbali za usimamizi wa kaunti. Miongoni mwa yaliojitokeza kwenye ripoti hio ni kuwa kaunti hio ina wafanyikazi hewa takriban 100, ambao wanapokea mishahara kila mwezi. Tayari wafanyikazi 24 wamesimamishwa kazi huku kaunti ikiahidi kutekeleza mapendekezo ya ripoti hio huku wahusika wakichukuliwa hatua za kisheria.