.
17th January, 2018
Mtoto mmoja amethibitishwa kufariki huku wengine wakiendelea kulazwa katika hospitali ya Tenwek kwa kile kinaaminika kuwa athari ya chanjo waliyopokea katika hospitali moja mjini Bomet. Kwa mujibu wa daktari wa watoto katika hospitali ya Tenwek, watoto hao wanne walifikishwa hospitalini wakiwa na uchungu na uvimbe kwenye maeneo waliyodungwa chanjo. Sasa serikali ya Bomet imelazimika kuahirisha utoaji chanjo uliopangiwa kufanyika ijumaa ili kutoa nafasi ya uchunguzi.