.
15th January, 2018
Kesi iliyokuwa ikipinga ushindi wa gavana wa taita taveta Granton Samboja imetupiliwa mbali na jaji wa mahakama kuu ya voi Eric Ogola. Jaji Ogola alisema kuwa kesi hiyo iliyowasilishwa na wapiga kura haikufikisha kiwango cha sheria kinachohitajika. Wafuasi wa samboja walifurahia uamuzi huo wa mahakama. Wafuasi hao walijaribu kuzuia gari la miguna miguna ambaye walitaka kujua sababu yake kuwa mahakamani. Aliyewasilisha kesi alikuwa ametilia shaka stakabadhi za elimu za Samboja. Samboja alichaguliwa katika uchaguzi wa agosti nane kwa Chama cha Wiper.