14th January, 2018
Wakazi wa eneo la Modogashe Kaunti ya Garissa sasa wana
kila sababu ya tabasamu baada ya kufunguliwa kwa shule ya
kwanza ya upili kwa wasichana. Kufunguliwa kwa shule hii
kumetoa matumaini makubwa kwa jamii hiyo ambayo
wasichana wengi wamekosa kujiunga na shule kutokana na
kuwepo kwa shule pekee ya upili inayojumuisha wanafunzi
wa kike na kiume.