13th January, 2018
Mtu mmoja amefariki huku maafisa wa polisi wanne wakijeruhi
baada ya wapiganaji wa alshabaab kushambulia msafara wa
mabasi uliokuwa ukielekea malindi na mombasa majira ya saa
tano hii leo. Kwa mujibu wa taarifa ya serikali kulikuwa
na makabiliano makali kati ya vikosi vya usalama vilivyokuwa
vikisindikiza mabasi hayo na wapiganaji hao. Wapiganaji hao
waliteketeza moto baadhi ya magari ya maafisa wa usalama.
seneta wa lamu anwar olei?tiptip amezungumzia kisa hicho
na kuvitaka vikosi vya usalama kuwa macho zaidi